Tuesday 20 October 2015

TIBA ILIYOTUKUKA: TIBA YA KISASA NA MATUMIZI MABAYA YA TIBA MBADALA


 TIBA ILIYOTUKUKA: TIBA YA KISASA NA MATUMIZI MABAYA YA TIBA MBADALA
Naandika hapa baada ya kuona hakuna anaeandika ama kujitokeza hadharani kuongelea kuhusu hili. Naamini kuna madaktari bingwa na wa uhakika wenye ujuzi mkubwa katika maswala yahusuyo tiba na afya kwa ujumla katika nchi hii; najua hawa ndio walipaswa waandike haya maana wana ujuzi na uzoefu zaidi yangu. Ila nahisi kwa uchache wao ukilinganisha na namba ya watu wanaohitaji huduma yao na kwa kujitolea kwao kwa ajili ya afya ya wengine wamebanana.
Mara kadhaa nikikaa mbele ya runinga ama kufungua redio huja vipindi vinavyojiita ni vya “afya”. Nami kwa kua ni mwanafunzi wa udaktari basi hujilamba midomo nisubiri elimu inayotolewa na watu waliokwenda kwenye mfumo huu wa kisasa wa mawasiliano ili wawafikie watanzania wengine kuwapa elimu ya afya na tiba. Hazipiti dakika chache baada ya kuanza kipindi huwa naanza kusikia maneno ya kuchefusha nikaukunja wangu wajihi, ila linalokuja kunitapisha huwa ni hawa watu wanaposema wana vibali vinavyotambulika na wizara ya afya na ustawi wa jamii.
Kwa kuwa natambua mtu anapohitaji tiba ama elimu ya kiafya huwa ana shida, shida hii huenda ikawa ugonjwa alionao ama kutaka kuzuia magonjwa ambayo bado hajayapata; Basi kimbilio la mnyonge huyu huwa ni wanaoitwa ama kujiita wataalam wa mambo ya afya ambao serikali kupitia wizara yake ya afya na ustawi wa jamii imewathibitisha ikawaruhusu wakaguse maisha ya watanzania. Hapa huwa siachi kufikiria jinsi kimbilio la wanyonge linavyoweza kujigeuza nyoka kwa kujikumbusha maneno ya mshairi T. Mvungi kwenye Mashairi ya Chekacheka:
Kimbilio la wanyonge, limejigeuza chatu,
Chatu mmeza matonge, asiyeogopa watu,
Dawaye uchonge singe, chatu afanywe si kitu,
Akishaoza samaki, busara ni kumtupa.
Naamini mimi ni mmoja kati ya watu wenye wajibu wa kuzichonga singe kumuokoa mtanzania mwenzangu kwenye janga hili la hawa watu na ninafanya hivyo kwenye haya chache zijazo:
Lakini kabla sijaenda mbali, na isijekua namie ninavutia upande wangu, kwanza tujiulize: NI IPI TIBA YA KWELI?
Tiba ya kweli ni ile iliyothibitishwa kufanya kile inachodai inafanya; iliyofanyiwa utafiti wa kina wa kisayansi usio baguzi. Hapa si tu ile anayopewa mtu alieugua tayari ili apone pekee bali ni pamoja na ushauri wowote wa kiafya unaotolewa (nakosa msamiati wa kuviunganisha hivi viwili). Hii ni ile ya kisasa ila baadhi ya tiba mbadala zimeoneshwa kuwa na vithibitisho pia, na hizi ni 1. Homeopathy (matumizi ya vitu vinavyosababisha ugonjwa kwa kiasi kidogo sana kutibu ugonjwa huo) 2. Osteopathy (kutibu kwa kutambua uhusiano kati ya misuli, mifupa na afya) 3. Chiropractic (kutibu kwa kutambua uhusiano kati ya uti wa mgongo na afya) 4. Acupuncture (kutuliza maumivu kwa kuchomeka sindano kwenye ngozi) 5. Herbal Medicine (mitishamba) (Davidson’s principles & practice of medicine 21st ed, 2010. Pg 15). Japo mara nyingi jinsi zinavyofanya kazi huwa inapotoshwa na kuzielezea moja baada ya nyingine itahitaji makala nyingine.
Acupuncture

Wengi wa hawa watu wanaokwenda kwenye runinga kufanya vipindi vya afya (ambavyo kiuhalisia huwa ni matangazo yao ya biashara) huwa wanaongea vitu wasivyovifaham kwa undani, ambavyo wana ujuzi navyo wa juu juu sana aidha kwa kusoma kwenye mitandao ama kusikia sehemu, ila cha muhimu kuliko yote ni kwamba havina VITHIBITISHO vya kisayansi kwa kile wanachosema. Nakumbuka wakati nipo sekondari nilikua navutiwa sana na habari za kisayansi, nilipenda kuzisikia ama kuziangalia kwenye runinga nyumbani. Alikuepo bwana mmoja aliitwa Isaac Ndodi aliekua akiendesha kipindi kilichoanza kwa nyimbo za dini na kisha akaanza kuelezea biolojia anayojua yeye mwenyewe na jinsi gani magonjwa yanatokea mfano alisema “kunywa maji pamoja na chakula husababisha magonjwa”. Nilipokua kitaaluma na nikawa naangalia nyuma niliwaza huyu bwana alikua anatoa wapi haya mambo? je alikua anatoa malezo yoyote kwanini? Je kulikua na vithibitisho vyovyote vya anavyodai? Na kama serikali ilimpa kibali kweli, je haifuatilii nini anafanya? Wengine walijitokeza wakisema wana dawa za kutibu magonjwa sugu kama kisukari, shinikizo la damu, saratani na kadhalika. Ila leo nikiwaza hawa walitakiwa wapate tuzo za nobel kwa kazi hizo.





Wengi wa hawa watu hupenda kuunganisha tiba zao na mambo ya kiroho. Watakwambia mungu aliwaweka wanadam wa kwanza wale mboga na matunda na wakaishi miaka mingi bila magonjwa; japo ukienda kwenye jamii zilizobaki zinazokula mboga na matunda mfano wahadzabe wa hapa kwetu utakuta wana afya mbovu zaidi yetu. Kitendo cha kuunganisha mambo ya kiroho na tiba zao ni mbinu za kumfanya mteja wao awaamini kiasi cha kutokuhoji kama tusivyotakiwa kuhoji mambo ya imani.
Na watu hawa wapo kwa ajili ya watu wenye pesa kwani huduma zao ni ghali mno tofauti na ilivyooneshwa kwenye mtandao wa Foreplan Herbal Clinic inayomilikiwa na J.J.Mwaka ambapo wanasema wao hawapo kwa ajili ya pesa bali huduma na mara nyingine hutoa huduma za bure kwa wasiojiweza. Ninae rafiki yake na rafiki yangu mmoja ambae amekua akisumbuliwa na maumivu ya mgongo kwa muda sasa na aliamua kujikita na hizi tiba mbadala na anasema baada ya yeye kuambiwa kushika kimtambo ambacho kinaweza “kuchunguza mwili mzima” basi walimwambia “wamegundua ana mafuta mengi kwenye mgongo na yanazuia damu inayopitia mgongoni isifike kwenye ubongo, hivyo ndio maana anaumwa mgongo”. Baadae wakamuuzia dawa za kienyeji ambazo alisema nyingine zilikua kama vumbi ambalo atakua anatia kwenye chai, na nyingine kama kinyesi cha ng’ombe, pia wakamshauri akanunue asali mbichi nyingi sana atumie na kwa wakati huo aache kula nyama kwani ina mafuta. Kwa vyote hivi alitumia zaidi ya Sh. 120,000/= za kitanzania na asione maumivu hata yakipungua wakati akikosa burudani ya vyakula vitamu vyenye protini nyingi kama nyama na kunyweshwa takataka asizozijua kwa dozi isiyochunguzwa madhara yake. Gharama hii kubwa husababisha hawa jamaa waone wagonjwa wachache kwa siku ukilinganisha na daktari wa tiba ya kisasa na ya kisayansi. Hapa huweza kuongea na wagonjwa kwa ukaribu sana na ujaliji ambao hata mimi ninautamani sana. Hiki ndicho huwa kinawaponya hawa wagonjwa ikitokea wanapona ukijumlisha na ukweli kwamba mwili una uwezo wake wa asili wa kujiponya wenyewe, na sio yale wanayoyafanya.
Ukienda kwenye tiba ya kisasa, achilia mbali usumbufu utakaoupata mwanzoni ili uonane na daktari pia hatoweza kukusikiliza kana kwamba upo peke yako siku iyo bali ni watu wengi waliozidi watu anaotakiwa kuwaona kwa siku ila nae hujitahidi kadiri awezavyo. Baada ya kukusikiliza hukumbuka kile alichojifunza ambacho njia za kisayansi dunia nzima zimeonesha hivyo, huja na hisia ya nini kinachokusumbua. Yeye haishii hapa bali hutaka kuonesha vithibitisho kama kweli anachofikiria ni sawa, na hapa atakuchukua vipimo (mfano atahitaji kujua kama kuuma kwa tumbo lako kunasababishwa na vijidudu vilivyokuingia tumboni pale ulipokula chakula kisicho salama, kwa kuchukua kinyesi chako na kupeleka maabara ili wakaangalie kama hivyo vijidudu vimo maana kinyesi kimetoka huko viliko vijidudu). Baadae akishajua nini shida hujiuliza ni njia gani ya kutibu ugonjwa wako inayotumika kwa sasa na ambayo imethibitishwa kisayansi na inakubalika dunia nzima. Basi utapewa dawa ama kufanyiwa upasuaji. Dawa zetu hawa jamaa wameziita kemikali pasi hata na kujua nini maana ya hili neon. Kemia ya kidato cha kwanza haikueleweka vizuri hapa. Kwa maana ya kemikali, zetu ni kemikali ila na zao ni kemikali, bila kusahau vitu vingi tu vya asili. Lakini siku zote mambo hayawi hivi kwani si magonjwa yote tunajua sababu zake; ila hata kama ikiwa hivyo tunakua wawazi tu na tunasubiri tukijua tafiti zinaendelea na ipo siku watakuja na majibu hata kama sisi tutakua hatupo.
Kwa kuhitimisha naomba nihimize mambo kadhaa:
Kwanza pindi tusikiapo watu wanatoa elimu za afya, tuwahoji watuelezee kwa kina tuelewe angalau kwa ujumla, kama hawawezi kutuelezea tuelewe basi wao wenyewe hawavielewi. Pili watupe vithibitisho vya kisayansi kuhusu yale wanayodai, watuambie wametoa wapi wanavyosema na kama wameota kama babu wa Loliondo basi tuwapotezee. Tatu tuwe wagumu wa kuamini haraka kama alivyokua Tomaso mwanafunzi wa Yesu; Tukisikia mtu anatibu saratani ama VVU/UKIMWI basi tujiulize kwa nini anakuja kuhangaika kwenye runinga ya ndani ya nchi wakati ugonjwa huo unatesa dunia nzima? Tujiulize kama hivyo vyakula wanavyosema vinatibu magonjwa flani mfano tango, nyanya, ukwaju, vitunguu na vinginenyo ni kwanini basi tunapata wakati twavila mara kwa mara? Mwisho tuunganishe nguvu kwa pamoja katika kuhimiza umuhimu wa kujielimisha na kukuza sekta ya afya ya kisasa maana hii ndiyo iliyoweza kuongeza muda wa wanadamu kuishi duniani maradufu, imeupoteza ugonjwa wa Ndui kwenye uso wa dunia kwa chanjo, imepunguza vifo vya watoto chini ya miaka 5 ukilinganisha na zamani, na haijakaa kibiashara kwani madaktari walio wengi huwa na wito wa kusaidia na wanaishi wakijua hawawezi kuwa matajiri, na mengine mengi.

JOSEPH JULIUS


Friday 14 August 2015

AJALI YA KIHISTORIA: RANGI, UWEZO WA KIAKILI NA TOFAUTI YA MAENDELEO DUNIANI


 
AJALI YA KIHISTORIA: RANGI, UWEZO WA KIAKILI NA TOFAUTI YA MAENDELEO DUNIANI

Tukiwa tumepumzika kwenye kivuli ikiwa ni baada ya vipindi vya darasani, tulijikuta katika mabishano ya kwa nini watu weupe wanaonekana kua wameendelea zaidi ya weusi. Wote walikubaliana kwamba watu weupe ni watofauti sana na ndivyo walivyozaliwa kua wenye akili na ndio maana wao waliwahi kuendelea hata wakaja kututawala na kutufanya watumwa. Katika lile kundi la takribani watu kumi na tano nikajikuta ni peke yangu tu ambae nilikua kinyume nao.
Lakini kama unavyojua, ubishi mwingi usiokua na mpangilio huwa hauangalii nani anasema nini ila wale wenye uwezo wa kupaza sauti ya juu na wanaokua wengi ndio huonekana wameshinda. Swali kama hili nilikua nalo kitambo sana hata kabla ya kukutana na haya mabishano. Ni mpaka pale nilipokutana na kitabu “Guns, Germs and Steel” ambapo mwandishi Jared Diamonds anaonesha kwa nini sehemu nyingine zilianza kuendelea kabla ya nyingine, ndipo angalau niliweza kujibiwa. Nami basi mamlaka yangu atakua Jared katika kulielezea hili.
Naomba nianze na kwa nini hawa wenzetu ni weupe kwa maksudi kabisa maana kwenye yale mabishano yetu ya kivulini mmoja kati yetu alikwenda mbali sana na kudiriki kusema kwamba “kile kinasaba kilichokuja na ile rangi nyeupe ndicho pia kitakua na uwezo wa kiakili wa hawa watu”. Lakini sayansi inatuambia sio hivyo. Tukumbuke vinasaba vyote vya mwanadam vinajulikana ikiwa ni mafanikio ya “Human Genome Project” iliyokamilika mwaka 2003 huko USA.
Tukumbuke watangulizi wa wanadamu walitoka afrika. Ni pale walipoanza kjifunza kutembea kwa miguu miwili ndipo walipoanza kuondoka afrika na kwenda kwingineko. Rangi nyeusi ndio rangi asilia ya watangulizi wetu. Watangulizi wetu walipoweka makazi kaskazini mwa ulaya ambako hakuna jua la kutosha, ngozi zao hazikuweza kufyonza kiasi cha jua la kutosha ili kupata vitamin D. Wengi walipata matatizo ya mifupa ikiwemo matege na haikua rahisi kwao kuzaa (aidha walifariki wao ama/na watoto wao wakati wa kujifungua ). Wakati huohuo mabadiliko yalitokea kwenye vinasaba vinavyohusika na utoaji wa rangi nyeusi (wanasayansi wamevigndua na kuviita SLC24A5 ) na kuwapa rangi nyeupe yenye uwezo wa kuingiza kiasi kikubwa cha jua lile chache. Kwahiyo wale waliokua wamepata mabadiliko kwenye vinasaba hivyo waliweza kuzaa vizuri na kuendeleza uzao wakati wengine wakitoweka, na ndio maana leo tunawaona ni weupe na sisi ni weusi, na hakuna chochote cha kushangaza kwenye rangi yao na aihusiani na wao kua na akili.
Picha: kuonesha kusambaa kwa watu kutoka afrika kwenda sehemu mbalimbali duniani
 
Kwanini wao waliendelea kabla yetu kiasi cha kututawala na kutufanya watumwa? Kwanza nianze kwa kusema hata kama tutabishana kuhusu jibu la swali hili, jibu la kwamba wao wana akili zaidi yetu hilo si kweli na hakuna vithibitisho vya hilo. Wanaopendelea jibu hilo mara nyingi ni wabaguzi wa rangi na wamefanikiwa kuingiza mawazo yao yasiyokua na vithibitisho kwenye bongo za wengi ikiwemo wale wote niliojikuta nao kivulini kwenye ubishi. Diamond anatuambia Wanasaikolojia kwenye nchi zenye mchanganyiko wa watu weupe na weusi wametafuta kwa nguvu zote kwa makumi ya miaka kuweza kuthibitisha kwamba watu weupe wana uwezo mkubwa wa kiakili ukilinganisha na weusi ila wasipate wanachotafuta. Wanawalinganisha watu bila hata kujiuliza kwamba wamekulia katika mazingira,tamaduni na wenye elimu tofauti. Jared Diamond mwenyewe ambae ameishi na watu wa New Guinea kwa miaka 33 akifanya tafiti zake anaamini wazawa wa New Guinea ni wenye akili zaidi ya wazungu wenzie kwa kuweza kuishi kwenye mazingira magum kama yale.
Kabla ya miaka 11,000 iliyopita watu wote duniani waliishi kwa kuwinda na kukusanya matunda na mizizi, hivyo katika kipindi hiki wote duniani tulifanana hali. Karibia Dunia nzima leo haipo huko tena isipokua kwa maeneo machache sana wakiwemo wahadzabe wa hapa Tanzania ambao naamini nao kadiri muda unavyokwenda watatoka huko. Ni mpaka miaka 11,000 iliyopita ndipo tulianza kutofautiana kwa kilimo kugunduliwa katika baadhi ya maeneo duniani. Kilimo ni muhimu katika swali letu maana jamii Fulani ikiachana na kuwinda na kula matunda na mizizi ikaanza kulima chakula na kukitunza kinachobaki na pia ikaanza kufuga na wanyama, kwanza jamii hii itaongezeka katika idadi ya watu, pili itapata maambukizi ya vijidudu vipya kutoka kwa wanyama wanaowafuga na mimea wanayootesha; na tatu kwa wingi wa jamii hii itawalazimu kutengeneza serikali na itakua na jeshi;watu mbalimbali watajikita katika shughuli tofautitofauti mbali na ile ya wawindaji na wakusanyaji ambamo wote huzunguka kutafuta chakula, katika jamii inayolima na kufuga wengine watajihusisha na kuendeleza teknolojia na humo zitatoka mashine kwa ajili ya kurahisisha kazi na silaha kwa ajili ya kutawala jamii nyingine. Pia watakapoenda kukutana na jamii nyingine ambayo ni mpya kwao wataiambukiza magonjwa ambayo wao tayari wana kinga nayo, nayo inaweza hata kutoweka. Hivyo wataishia kuwatawala wale ambao hawakuwa/walichelewa kuanza kilimo. Vithibitisho vilivyopo mpaka leo vinaonesha kilimo kilianza kwa mara ya kwanza katika maeneo matano duniani ambayo ni: kusini magharibi mwa asia (pia hujulikana kama mashariki ya karibu); China; Mesoamerica (yaani mexico ya kati na kusini na maeneo ya karibu na amerika ya kati); Andes ya amerika kusini; na mashariki mwa marekani.
Lakini hapa tumeongeza swali lingine kubwa zaidi, kwanini kilimo na ufugaji ugunduliwe miaka11,000 iliyopita kwao kwanza na si huku? Jibu lake sio kwa kua babu zao walikua na akili sana kuzidi babu zetu hapana ila ni “ajali ya kihistoria” kama Diamond mwenyewe anavyoiita. Maana yake ni kwamba ilitokea kama ajali wao wakajikuta wapo katika maaeneo ambayo yanaruhusu kuanzisha kilimo na ufugaji tofauti na sisi. Nitatoa mifano kadhaa:
Asia na ulaya kwa pamoja inaitwa “Eurasia” na imeungana, ni kubwa zaidi katika latitudo kuliko longitudo. Hii inamaanisha kuna mabadiliko ya tabia nchi kwa kiasi kidogo ukilinganisha na mabara ambayo ni makubwa katika longitudo mfano afrika. Hii husaidia kuweza kusambaa kwa urahisi kwa mimea na mifugo kutoka sehem moja kwenda nyingine kwa sababu wanakua wamezoea mazingira yaleyale. Pia eneo kubwa kabisa la kimediterania duniani linapatikana magharibi mwa “Eurasia”; eneo hili lina mtawanyiko mkubwa wa mimea na wanyama, linafaa kwa kilimo na ufugaji.
Eurasia” ndiko chanzo cha mazao mengi ya kilimo na wanyama wengi wanaoonekana leo duniani wakifugwa. Kati ya mifugo mikuu mitano ya kufuga iliyopo duniani leo, minne (ng’ombe, mbuzi, kondoo na nguruwe) ilifugwa kwa mara ya kwanza huko na baadae kutawanywa maeneo mbalimbali duniani.
Kwa kua chakula kilipatikana kwa wingi katika meeneo yaliyoanza kulima hata kingine kikatunzwa. Hakukua na haja ya kila mtu kujikita katika utafutaji wa chakula. Basi watu wakabobea katika fani mbalimbali. Wengine wakawa viongozi wa serikali wenye kuangalia wapi pa kutawala na kuendesha jamii kupitia kodi iliyokua ikikusanywa. Wengine wakawa wanajeshi na kupigana katika vita vya kuyatawala maeneo mengine yaliyokua hayajaendelea. Wenngine wakajikita na teknolojia wakatengeneza mashine mbalimbali kama magari ya kuvutwa na farasi, silaha zenye uwezo wa hali ya juu kama bunduki ukilinganisha na mawe ama marungu waliokua nayo waliopambana nao. Na kikubwa zaidi wakagundua kuandika, kitu ambacho kiliharakisha utawala wa maeneo mapya pale walipoyaona na kuandika kuhusu taarifa zake na habari zikawafikia wengine katika maeneo mengine.
Kuhitimisha, ni kwamba hawa watu weupe walianza kuendelea kabla ya wengine sio kwa sababu wao wana akili sana ama wamebarikiwa sana ila ni kama bahati kwao kwamba walijikuta katika maeneo ambako kuna uwezekano wa kuendelea kuliko mengine, maeneo yenye wanyama wa kufugika, yenye mimea ya kufanyia kilimo na yenye geografia inayoruhusu. Kama tungekua tumekwishagundua chombo chenye uwezo wa kurudi nyuma ya muda (time machine) na tungerudi miaka 11,000 iliyopita tukabadilisha sisi ndio tukaanza kugundua kilimo na ufugaji na wao wakaendelea kua wawindaji na wakusanya matunda na mizizi, leo ingekua kinyume na ilivyo. Kwa leo kila wanachoweza kufanya hata sisi tunaweza kama tumepewa kile walichopewa ili wafanye kitu flani mfano elimu ama mtaji. Wenzetu wanaoishi nao katika maazingira yaleyale wamekwishatuonesha vithibitisho kwa kufanya vitu vikubwa huko kwao. Obama, Dr. Ben Carson, Martin Luther King, Nelson Mandela, Kambarage Nyerere, Kofi Annan, Wangari Muta Maathai, Oprah Winfrey ni mifano michache tu.

Tujiamini na tuongeze bidii ya kubadilisha hali ya jamii yetu, tusikubali mawazo ya kiubaguzi wa rangi kuzama kwenye maada yenye kilo 2 iliyokaa ndani ya mafuvu yetu, uliokuwepo ni utofauti wa kimazingira na sio vitu ambavyo vipo ndani yetu. 

Joseph J. Masalu
Muhimbili University of health and allied sciences(MUHAS)

Saturday 3 January 2015

will you be able to eat printed meat? printed blood vessel and organs-a breakthrough in medical field.

Imagine if you are eating meat which has been made from scratch - without slaughtering any animal. Will you be able to feel the taste of it?
Modern Meadow believes it can do just that - by making artificial raw meat using a 3D bioprinter.[1]
The Modern Meadow applies the latest advances in tissue engineering to develop novel biomaterials to address some of our most pressing global challenges. We develop cultured leather and meat products which require no animal slaughter and much lower inputs of land, water, energy and chemicals.[2]
For three-dimensional printing, solid objects are made from a digital model. It's also known as additive manufacturing: to make the structure tiny droplets are "printed" - layer by layer - via a carefully controlled inkjet nozzle.
The principle has been around for more than a decade, and is already used successfully to create jewellery, toys, furniture, cars, and even - most recently - parts of a gun.
Some researchers have also managed to print food like chocolate.
To bioengineer meat, the scientists first get stem cells or other specialised cells from an animal via a common procedure known as biopsy.
Stem cells are cells able to replicate themselves many times, and also can turn into other specialised cells. Once the cells multiplied to sufficient numbers, they are put into a bio-cartridge.
So instead of traditional ink or a material like plastic, the 3D printer cartridge contains something called bioink made of hundreds of thousands of live cells.
Once printed in the desired shape, the bioink particles naturally fuse to form living tissue.
This process of bioprinting biomaterials is similar to attempts to print artificial organs for transplants -the organovo
Although the actual process of making meat may be simpler, it will be challenging to produce such meat on an industrial scale, and persuade consumers to accept it.
So in the future, more cows may be able to roam the fields without having to fear the slaughterhouse.
This technology will be helpfull in famine countries.

ORGAN BIOPRINT
Oganovo is a company based in San Diego, California.
Organovo designs and creates multi-cellular, dynamic and functional human tissues for use in drug discovery and medical research. Our proprietary 3D bioprinting technology enables the creation of tissues that mimic key aspects of native tissues.
Organovo’s tissues are made available through testing services, customized projects, partnerships, and eventual therapeutic applications.
Their latest science invention is a technology (novogen) which allows living tissue cells to be assembled into patterns and complex structures, such as organs.
Organovo has partnered with other companies to develop a bio-printer.The device prints (places) human cells in a three-dimensional matrix to construct human tissue.
Currently, the bio-printer can grow blood vessels. It is anticipated that within five years the device will construct arteries and by 2020 sophisticated organs will be built by the device.
In 2010, Organovo successfully bioprinted functional blood vessels made from the cells of an individual person.
This is breakthrough in medical field,many diseases like vasicular diseases can be treated and cured.



REFERENCE :
http://m.bbc.com/news/technology-20972018
http://modernmeadow.com/
http://www.organovo.com/